All Businesses

Dar es Salaam · Business Profile

MASASI FARMING AND AGRO BUSINESS

Est. 2017
2017
Established
0
Products
Madale mwisho
Operating Zone
📋 About This Business

Consultation


TUNATENGENEZA GREENHOUSE NA NETHOUSE PAMOJA NA KUKUPATIA MICHE YA ZAO LOLOTE LILE LA MBOGA MBOGA KAMA NYANYA, PILIPILI HOHO NA MBOGA MBOGA KWA GHARAMA NAFUU,

Tunatengeneza greenhouse za ukubwa tofauti kutokana na eneo husika,

a) tunajenga za miti, ambazo hukaa kwa muda wa miaka 8,

a) mita 6 upana 12 urefu,tunajenga tunalifunika kwa wavu maalum, ambayo kazi yake ni kuweka uwiano sawa wa hali ya hewa inayofaa kwa mimea,, gharama yake milioni 3.5

1, mita 8 upana na mita 15 ni urefu, tunajenga tunalo funika kwa wavu maalum, ambapo ndani yake tunaweka miche 400 inaweza kuwa nyanya au pilipili hoho za rangi tofauti kama njano na nyekundu, tunaweka mfumo wa umwagiliaji maji, tank la maji lita elfu moja, kwa gharama ya milion 5.

2. Mita 8 upana na mita 25 urefu, tunajenga banda kuweka wavu maalum, tunaweka mfumo wa umwagiliaji maji, tunakupatia miche mia 800, ya zao utakalohitaji kama nyanya, pilipili hoho za rangi tofauti kama njano na nyekundu, tank la maji la lita elfu 1000 gharama yake ni milioni 7.

3. Mita 10 upana 30 urefu , tunajenga banda tunaloweka wavu maalum, tunaweka mfumo wa umwagiliaji maji, tunakupatia miche 1200, ya zao utakalolihitaji kama nyanya au pilipili hoho za rangi, tunaweka tank la kuhifadhia maji la lita elfu 2000, kwa gharama ya milioni 11.

Katika hii miradi ya greenhouse kuna pande mbili mteja na ofisi hivyo mteja anapaswa kufanya yafuatayo -

1. Kutoa fedha kwaajili ya mradi husika kutokana na size atakayohitaji,

2. Kuandaa eneo la mradi liwe safi na pia kuandaa chanzo cha maji,

3. Kununua au kuandaa mbolea ya samadi,

4. Kununua kamba na waya kwaajili ya kufanya ropping.

Majukumu ya ofisi kwa mteja -

1. Kujenga jengo la greenhouse ambalo linawekwa wavu, mfumo wa umwagiliaji( drip )

2. Kutoa miche na kupanda miche katika greenhouse,

3. Kufanya installation ya drip na bomba katika tank,

4. Kutoa ushauri wa mimea na kusaidia katika utafutaji masoko.

Namna sahihi ya uhudumiaji wa greenhouse hasa mazao yakishawekwa shambani ni kama ifuatavyo

1. Kuhakikisha miche inapata maji kwa wakati kila asubuhi na jioni nyakati za asubuhi maji yafunguliwe kwa muda wa lisaa limoja na jioni pia lisaa limoja.

2. Kuhakikisha miche inapigwa dawa katika muda utakaopangwa.

3. Kufanya mawasiliano na wataalam kila mara katika kujua maendeleo ya mradi. 

NB: Bei hizi ni kwa mirunda au miti

Kwa mawasiliano zaidi tupigie *0745478823, 0657570212*

📍
Office Zone Madale mwisho
🏢
Address SLP 67225
Listed Products 0 products
🛍️

No Products Listed Yet

This business hasn't added anything to their catalog yet.